Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 19:6-13 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Mifereji yake itatoa uvundo,vijito vyake vitapunguka na kukauka.Nyasi na mafunjo yake yataoza.

7. Sehemu za kandokando ya Nili zitakuwa tupu.Mimea yote iliyopandwa humo itakaukana kupeperushiwa mbali na kutoweka.

8. Wavuvi watalia na kuomboleza,wote watumiao ndoana watalalama;wote wanaotanda nyavu majini watakufa moyo.

9. Wafuma nguo za kitani watakata tamaa,wote kwa pamoja watakufa moyo.

10. Wafuma nguo watafedheheshwa,na vibarua watahuzunika.

11. Viongozi wa mji wa Soani ni wapumbavu kabisa,washauri wa Farao wanatoa shauri la kijinga!Awezaje kila mmoja kumwambia Farao,“Mimi ni mzawa wa mtaalamu stadi;mzawa wa wafalme wa hapo kale!”

12. Wako wapi, ewe Farao, wataalamu wako?Waache basi wakuambie na kukujulishaaliyopanga Mwenyezi-Mungu wa majeshi dhidi ya Misri!

13. Lakini viongozi wa Soani ni wapumbavu,wakuu wa Memfisi wamedanganyika.Hao walio msingi wa makabila yaowamelipotosha taifa la Misri.

Kusoma sura kamili Isaya 19