Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 19:5-10 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Maji ya mto Nili yatakaushwa,nao utakauka kabisa.

6. Mifereji yake itatoa uvundo,vijito vyake vitapunguka na kukauka.Nyasi na mafunjo yake yataoza.

7. Sehemu za kandokando ya Nili zitakuwa tupu.Mimea yote iliyopandwa humo itakaukana kupeperushiwa mbali na kutoweka.

8. Wavuvi watalia na kuomboleza,wote watumiao ndoana watalalama;wote wanaotanda nyavu majini watakufa moyo.

9. Wafuma nguo za kitani watakata tamaa,wote kwa pamoja watakufa moyo.

10. Wafuma nguo watafedheheshwa,na vibarua watahuzunika.

Kusoma sura kamili Isaya 19