Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 14:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawateua tena Waisraeli. Atawarudisha katika nchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.

2. Watu wa mataifa watawasaidia Waisraeli kurudi katika nchi waliyopewa na Mwenyezi-Mungu. Na hapo watawatumikia Waisraeli kama watumwa. Wale waliowateka sasa watatekwa na Waisraeli, na watawatawala wale waliowadhulumu.

3. Ewe Israeli, wakati Mwenyezi-Mungu atakapokufariji baada ya mateso, misukosuko na utumwa uliofanyiwa,

4. utaimba utenzi huu wa kumdhihaki mfalme wa Babuloni:“Jinsi gani mdhalimu alivyokomeshwa!Ujeuri wake umekomeshwa!

5. Mwenyezi-Mungu amelivunja gongo la waovu,ameivunja fimbo ya kifalme ya watawala,

6. ambao walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma,na kuwatawala kwa udhalimu bila huruma.

Kusoma sura kamili Isaya 14