Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 14:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawateua tena Waisraeli. Atawarudisha katika nchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.

2. Watu wa mataifa watawasaidia Waisraeli kurudi katika nchi waliyopewa na Mwenyezi-Mungu. Na hapo watawatumikia Waisraeli kama watumwa. Wale waliowateka sasa watatekwa na Waisraeli, na watawatawala wale waliowadhulumu.

3. Ewe Israeli, wakati Mwenyezi-Mungu atakapokufariji baada ya mateso, misukosuko na utumwa uliofanyiwa,

4. utaimba utenzi huu wa kumdhihaki mfalme wa Babuloni:“Jinsi gani mdhalimu alivyokomeshwa!Ujeuri wake umekomeshwa!

5. Mwenyezi-Mungu amelivunja gongo la waovu,ameivunja fimbo ya kifalme ya watawala,

6. ambao walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma,na kuwatawala kwa udhalimu bila huruma.

7. Sasa dunia yote ina utulivu na amani,kila mtu anaimba kwa furaha.

8. Misonobari inafurahia kuanguka kwako,nayo mierezi ya Lebanoni pamoja yasema:‘Kwa vile sasa umeangushwa,hakuna mkata miti atakayekuja dhidi yetu!’

9. “Kuzimu nako kumechangamka,ili kukulaki wakati utakapokuja.Kunaiamsha mizimu ije kukusalimuna wote waliokuwa wakuu wa dunia;huwaamsha kutoka viti vyao vya enziwote waliokuwa wafalme wa mataifa.

10. Wote kwa pamoja watakuambia:‘Nawe pia umedhoofika kama sisi!Umekuwa kama sisi wenyewe!

Kusoma sura kamili Isaya 14