Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 11:7-14 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Ngombe na dubu watakula pamoja,ndama wao watapumzika pamoja;na simba atakula majani kama ng'ombe.

8. Mtoto mchanga atacheza kwenye shimo la nyokamtoto ataweza kutia mkono shimoni mwa nyoka wa sumu.

9. Katika mlima mtakatifu wa Munguhakutakuwa na madhara wala uharibifu.Maana kumjua Mwenyezi-Mungu kutaenea pote nchini,kama vile maji yajaavyo baharini.

10. Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa ishara kwa mataifa; mataifa yatamtafuta na makazi yake yatatukuka.

11. Siku hiyo, Bwana ataunyosha mkono wake tena kuwarejesha watu wake waliosalia huko Ashuru, Misri, Pathrosi, Kushi, Elamu, Shinari, Hamathi na sehemu za pwani.

12. Naye atatweka bendera kuwaashiria mataifa,kuwakusanya Waisraeli waliodharauliwa,kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa,na kuwarudisha toka pembe nne za dunia.

13. Wivu wa Efraimu juu ya Yuda utakoma,hakutakuwa tena na uadui kati ya Yuda na Efraimu.

14. Wote pamoja watawavamia Wafilisti walio magharibi,pamoja watawapora watu wakaao mashariki.Watawashinda Waedomu na Wamoabu,nao Waamoni watawatii.

Kusoma sura kamili Isaya 11