Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 11:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kutatokea chipukizi katika kisiki cha Yese,tawi litachipua mizizini mwake.

2. Roho ya Mwenyezi-Mungu itakaa kwake,roho ya hekima na maarifa,roho ya shauri jema na nguvu,roho ya ujuzi na ya kumcha Mwenyezi-Mungu.

3. Atafurahia kumcha Mwenyezi-Mungu.Hatahukumu kadiri ya mambo ya njenje,wala kuamua kufuatana na yale anayosikia.

4. Atawapatia haki watu maskini,atawaamulia sawasawa wanyonge nchini.Kwa neno lake ataiadhibu dunia,kwa tamko lake atawaua waovu.

5. Haki itakuwa kama mkanda wa kujifunga,uaminifu utakaa naye kama mkanda kiunoni.

6. Mbwamwitu ataishi pamoja na mwanakondoo,chui watapumzika pamoja na mwanambuzi.Ndama na wanasimba watakula pamoja,na mtoto mdogo atawaongoza.

7. Ngombe na dubu watakula pamoja,ndama wao watapumzika pamoja;na simba atakula majani kama ng'ombe.

Kusoma sura kamili Isaya 11