Agano la Kale

Agano Jipya

Hosea 9:5-13 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mtafanya nini katika sikukuu ile iliyopangwa,au katika karamu ya Mwenyezi-Mungu?

6. Mtakapoyakimbia maangamizi ya nchi yenu,Misri itawakaribisheni kwake,lakini makaburi yenu yawangoja huko Memfisi.Magugu yatamiliki hazina zenu za fedha,miiba itajaa katika mahema yenu.

7. Siku za adhabu zimewadia,naam, siku za kulipiza kisasi zimefika;Waisraeli lazima wautambue wakati huo!Nyinyi mnasema, “Nabii ni mpumbavu;anayeongozwa na roho ni mwendawazimu.”Mnasema hivyo kwa sababu ya uovu wenu mkubwa,kwa sababu ya chuki yenu kali dhidi yake.

8. Nabii ni mlinzi wa Waefraimu kwa niaba ya Mungu;lakini, kokote aendako anategewa mtego kama ndege.Hata nyumbani mwa Mungu wake anachukiwa.

9. Nyinyi mmezama katika uovu,kama ilivyokuwa kule Gibea.Mungu atayakumbuka makosa yao,na kuwaadhibu kwa dhambi zao.

10. Mwenyezi-Mungu asema:“Nilipowakuta Waisraeliwalikuwa kama zabibu jangwani.Nilipowaona wazee wenuwalikuwa bora kama tini za kwanza.Lakini mara walipofika huko Baal-peori,walijiweka wakfu kuabudu chukizo Baali,wakawa chukizo kama hicho walichokipenda.

11. Fahari ya Efraimu itatoweka kama ndege;watoto hawatazaliwa tena,hakutakuwa na watoto wa kuzaliwa,wala hakutakuwa na kuchukuliwa mimba!

12. Hata kama wakilea watoto,sitamwacha hai hata mmoja wao.Ole wao, nitakapowaacha peke yao!”

13. Kama nilivyokwisha ona hapo kwanza,Efraimu alikuwa kama mtende mchanga penye konde zuri;lakini sasa Efraimu itamlazimu kuwapeleka watoto wake wauawe.

Kusoma sura kamili Hosea 9