Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 13:23-26 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Walipofika katika Bonde la Eshkoli, watu hao walikata shada la mzabibu lililokuwa na matunda mengi nalo lilibebwa na watu wawili juu ya mti. Walichukua pia makomamanga kadhaa na tini.

24. Mahali hapo paliitwa Bonde la Eshkoli kwa sababu ya shada ambalo watu hao wa Israeli walikata kutoka mahali hapo.

25. Baada ya kuipeleleza nchi kwa muda wa siku arubaini, watu hao walirudi.

26. Waliwaendea Mose, Aroni na jumuiya ya Waisraeli huko Kadeshi, katika jangwa la Parani, wakatoa taarifa ya mambo waliyoyaona na kuwaonesha matunda ya nchi.

Kusoma sura kamili Hesabu 13