Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 11:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Watu walianza kumlalamikia Mwenyezi-Mungu juu ya taabu zao. Mwenyezi-Mungu aliposikia, alishikwa na hasira, akawapelekea moto. Moto huo uliwaka kati yao na kuchoma upande mmoja wa kambi.

2. Watu wakamlilia Mose, naye akamwomba Mwenyezi-Mungu na moto huo ukazimika.

3. Kwa hiyo, mahali hapo pakaitwa Tabera, kwa sababu hapo moto wa Mwenyezi-Mungu uliwaka kati ya watu.

4. Miongoni mwa Waisraeli kulikuwa na kundi fulani lililoandamana nao ambalo lilikuwa na hamu kubwa. Waisraeli kwa mara nyingine walilia, wakisema. “Laiti kama tungeweza kupata nyama ya kula!

5. Tunakumbuka, samaki tuliokula kule Misri bila malipo, matango, matikiti, mboga, vitunguu na vitunguu saumu!

6. Lakini sasa nguvu zimetuishia na hakuna chakula kingine isipokuwa hii mana tu!”

Kusoma sura kamili Hesabu 11