Agano la Kale

Agano Jipya

Habakuki 3:6-18 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Akisimama dunia hutikisika;akiyatupia jicho mataifa, hayo hutetemeka.Milima ya milele inavunjwavunjwa,vilima vya kudumu vinadidimia;humo zimo njia zake za kale na kale.

7. Niliwaona watu wa Kushani wakiteseka,na watu wa Midiani wakitetemeka.

8. Ee Mwenyezi-Mungu, je, umeikasirikia mito?Je, umeyakasirikia maji ya bahari,hata ukaendesha farasi wako,na magari ya vita kupata ushindi?

9. Uliuweka tayari uta wako,ukaweka mishale yako kwenye kamba.Uliipasua ardhi kwa mito.

10. Milima ilikuona, ikanyauka;mafuriko ya maji yakapita humo.Vilindi vya bahari vilinguruma,na kurusha juu mawimbi yake.

11. Jua na mwezi vilikaa kimya katika makazi yao,vilipoona miali ya mishale yako ikienda kasi,naam, vilipouona mkuki wako ukimetameta.

12. Kwa ghadhabu ulipita juu ya nchi,uliyakanyaga mataifa kwa hasira yako.

13. Ulitoka kwenda kuwaokoa watu wako,kumwokoa yule uliyemweka wakfu kwa mafuta.Ulimponda kiongozi wa jamii ya waovu,ukawaangamiza kabisa wafuasi wake.

14. Amiri jeshi ulimchoma mishale yako,jeshi lilipokuja kama kimbunga kututawanya,wakijigamba kuwaangamiza maskini mafichoni mwao.

15. Kwa farasi wako ulitembea juu ya bahari,bahari inayosukwasukwa na mawimbi.

16. Nasikia hayo nami ninashtuka mwilini,midomo yangu inatetemeka kwa hofu;mifupa yangu inateguka,miguu yangu inatetemeka.Ninangojea kwa utulivu siku ile ya maafa,ambayo inawajia wale wanaotushambulia.

17. Hata kama mitini isipochanua maua,wala mizabibu kuzaa zabibu;hata kama mizeituni isipozaa zeituni,na mashamba yasipotoa chakula;hata kama kondoo wakitoweka zizini,na mifugo kukosekana mazizini,

18. mimi nitaendelea kumfurahia Mwenyezi-Mungunitamshangilia Mungu anayeniokoa.

Kusoma sura kamili Habakuki 3