Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3

Agano la Kale

Agano Jipya

Habakuki 3 Biblia Habari Njema (BHN)

Sala ya Habakuki

1. Sala ya nabii Habakuki:

2. Ee Mwenyezi-Mungu, nimesikia juu ya fahari yako,juu ya matendo yako, nami naogopa.Uyafanye tena mambo hayo wakati wetu;uyafanye yajulikane wakati huu wetu.Ukasirikapo tafadhali ukumbuke huruma yako!

3. Mungu amekuja kutoka Temani,Mungu mtakatifu kutoka mlima Parani.Utukufu wake umetanda pote mbinguni,nayo dunia imejaa sifa zake.

4. Mng'ao wake ni kama wa jua;miali imetoka mkononi mwakeambamo nguvu yake yadhihirishwa.

5. Maradhi yanatangulia mbele yake,nyuma yake yanafuata maafa.

6. Akisimama dunia hutikisika;akiyatupia jicho mataifa, hayo hutetemeka.Milima ya milele inavunjwavunjwa,vilima vya kudumu vinadidimia;humo zimo njia zake za kale na kale.

7. Niliwaona watu wa Kushani wakiteseka,na watu wa Midiani wakitetemeka.

8. Ee Mwenyezi-Mungu, je, umeikasirikia mito?Je, umeyakasirikia maji ya bahari,hata ukaendesha farasi wako,na magari ya vita kupata ushindi?

9. Uliuweka tayari uta wako,ukaweka mishale yako kwenye kamba.Uliipasua ardhi kwa mito.

10. Milima ilikuona, ikanyauka;mafuriko ya maji yakapita humo.Vilindi vya bahari vilinguruma,na kurusha juu mawimbi yake.

11. Jua na mwezi vilikaa kimya katika makazi yao,vilipoona miali ya mishale yako ikienda kasi,naam, vilipouona mkuki wako ukimetameta.

12. Kwa ghadhabu ulipita juu ya nchi,uliyakanyaga mataifa kwa hasira yako.

13. Ulitoka kwenda kuwaokoa watu wako,kumwokoa yule uliyemweka wakfu kwa mafuta.Ulimponda kiongozi wa jamii ya waovu,ukawaangamiza kabisa wafuasi wake.

14. Amiri jeshi ulimchoma mishale yako,jeshi lilipokuja kama kimbunga kututawanya,wakijigamba kuwaangamiza maskini mafichoni mwao.

15. Kwa farasi wako ulitembea juu ya bahari,bahari inayosukwasukwa na mawimbi.

16. Nasikia hayo nami ninashtuka mwilini,midomo yangu inatetemeka kwa hofu;mifupa yangu inateguka,miguu yangu inatetemeka.Ninangojea kwa utulivu siku ile ya maafa,ambayo inawajia wale wanaotushambulia.

17. Hata kama mitini isipochanua maua,wala mizabibu kuzaa zabibu;hata kama mizeituni isipozaa zeituni,na mashamba yasipotoa chakula;hata kama kondoo wakitoweka zizini,na mifugo kukosekana mazizini,

18. mimi nitaendelea kumfurahia Mwenyezi-Mungunitamshangilia Mungu anayeniokoa.

19. Bwana, Mwenyezi-Mungu ndiye nguvu yangu,huiimarisha miguu yangu kama ya paa,huniwezesha kupita juu milimani.