Agano la Kale

Agano Jipya

Habakuki 3:13-17 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Ulitoka kwenda kuwaokoa watu wako,kumwokoa yule uliyemweka wakfu kwa mafuta.Ulimponda kiongozi wa jamii ya waovu,ukawaangamiza kabisa wafuasi wake.

14. Amiri jeshi ulimchoma mishale yako,jeshi lilipokuja kama kimbunga kututawanya,wakijigamba kuwaangamiza maskini mafichoni mwao.

15. Kwa farasi wako ulitembea juu ya bahari,bahari inayosukwasukwa na mawimbi.

16. Nasikia hayo nami ninashtuka mwilini,midomo yangu inatetemeka kwa hofu;mifupa yangu inateguka,miguu yangu inatetemeka.Ninangojea kwa utulivu siku ile ya maafa,ambayo inawajia wale wanaotushambulia.

17. Hata kama mitini isipochanua maua,wala mizabibu kuzaa zabibu;hata kama mizeituni isipozaa zeituni,na mashamba yasipotoa chakula;hata kama kondoo wakitoweka zizini,na mifugo kukosekana mazizini,

Kusoma sura kamili Habakuki 3