Agano la Kale

Agano Jipya

Ezra 8:7-19 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Yeshaya, mwana wa Athalia, wa ukoo wa Elamu, pamoja na wanaume 70.

8. Zebadia, mwana wa Mikaeli, wa ukoo wa Shefatia, pamoja na wanaume 80.

9. Obadia, mwana wa Yehieli, wa ukoo wa Yoabu, pamoja na wanaume 218.

10. Shelomithi, mwana wa Yosifia, wa ukoo wa Bani, pamoja na wanaume 160.

11. Zekaria, mwana wa Bebai, wa ukoo wa Bebai, pamoja na wanaume 28.

12. Yohanani, mwana wa Hakatani, wa ukoo wa Azgadi, pamoja na watu 110.

13. Elifeleti, Yeueli na Shemaya, wa ukoo wa Adonikamu, pamoja na wanaume 60, (hawa walirudi baadaye).

14. Uthai na Zakuri, wa ukoo wa Bigwai, pamoja na wanaume 70.

15. Niliwakusanya pamoja watu wote kando ya mto uelekeao mji wa Ahava. Huko, tulipiga kambi kwa muda wa siku tatu. Niliwakagua watu wote pamoja na makuhani, lakini sikupata Walawi miongoni mwao.

16. Niliita waje kwangu viongozi tisa: Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu, pamoja na waalimu wawili, Yoyaribu na Elnathani.

17. Nikawatuma kwa Ido, kiongozi wa jamii ya watu kule Kasifia, nikimwomba yeye pamoja na wenzake wahudumu wa nyumba ya Mungu, watuletee watu watakaohudumu katika nyumba ya Mungu.

18. Kwa neema yake Mungu, walituletea Sherebia, mtu mwenye busara na Mlawi wa ukoo wa Mahli, pamoja na wanawe na ndugu zake kumi na wanane.

19. Walituletea pia Hashabia na Yeshaya, wote wa ukoo wa Merari, pamoja na ndugu zao ishirini.

Kusoma sura kamili Ezra 8