Agano la Kale

Agano Jipya

Ezra 8:1-17 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ifuatayo ni orodha ya viongozi wa koo za watu waliorudi pamoja nami Ezra kutoka Babuloni, wakati wa utawala wa mfalme Artashasta:

2. Gershomu, wa ukoo wa Finehasi. Danieli, wa ukoo wa Ithamari. Hatushi, wa ukoo wa Daudi,

3. aliyekuwa mwana wa Shekania. Zekaria, wa ukoo wa Paroshi, pamoja na wanaume 150 wa ukoo wake, walioandikishwa pamoja.

4. Eliehoenai, mwana wa Zerahia, wa ukoo wa Pahath-moabu, pamoja na wanaume 200.

5. Shekania, mwana wa Yahazieli, wa ukoo wa Zatu, pamoja na wanaume 300.

6. Ebedi, mwana wa Yonathani, wa ukoo wa Adini, pamoja na wanaume 50.

7. Yeshaya, mwana wa Athalia, wa ukoo wa Elamu, pamoja na wanaume 70.

8. Zebadia, mwana wa Mikaeli, wa ukoo wa Shefatia, pamoja na wanaume 80.

9. Obadia, mwana wa Yehieli, wa ukoo wa Yoabu, pamoja na wanaume 218.

10. Shelomithi, mwana wa Yosifia, wa ukoo wa Bani, pamoja na wanaume 160.

11. Zekaria, mwana wa Bebai, wa ukoo wa Bebai, pamoja na wanaume 28.

12. Yohanani, mwana wa Hakatani, wa ukoo wa Azgadi, pamoja na watu 110.

13. Elifeleti, Yeueli na Shemaya, wa ukoo wa Adonikamu, pamoja na wanaume 60, (hawa walirudi baadaye).

14. Uthai na Zakuri, wa ukoo wa Bigwai, pamoja na wanaume 70.

15. Niliwakusanya pamoja watu wote kando ya mto uelekeao mji wa Ahava. Huko, tulipiga kambi kwa muda wa siku tatu. Niliwakagua watu wote pamoja na makuhani, lakini sikupata Walawi miongoni mwao.

16. Niliita waje kwangu viongozi tisa: Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu, pamoja na waalimu wawili, Yoyaribu na Elnathani.

17. Nikawatuma kwa Ido, kiongozi wa jamii ya watu kule Kasifia, nikimwomba yeye pamoja na wenzake wahudumu wa nyumba ya Mungu, watuletee watu watakaohudumu katika nyumba ya Mungu.

Kusoma sura kamili Ezra 8