Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 7:15-27 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Nje kuna kifo kwa upangana ndani ya mji kuna maradhi mabaya na njaa.Walioko shambani watakufa kwa upanga;walio mjini njaa na maradhi mabaya yatawaangamiza.

16. Wakiwapo watu watakaosalimikawatakimbilia milimani kama hua waliotishwa bondeni.Kila mmoja wao ataomboleza kwa dhambi zake.

17. Kila mtu, mikono yake itakuwa dhaifuna magoti yake yatakuwa maji.

18. Watavaa mavazi ya gunia,hofu itawashika,nao watakuwa na aibu,vichwa vyao vyote vitanyolewa.

19. Watatupa fedha yao barabaranina dhahabu yao itakuwa kama kitu najisi.Fedha na dhahabu zao hazitaweza kuwaokoakatika siku hiyo ya ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu;wala hawataweza kushibaau kuyajaza matumbo yao fedha na dhahabu waliyojirundikia;kwani mali hiyo ndiyo chanzo cha dhambi yao.

20. Kwa kuwa walijifanyia utukufu usio na maana kwa njia ya vikuku,wakajifanyia sanamu za miungu zinazochukizapamoja na vitu vyao vya aibu;vyote hivyo nitavifanya kuwa najisi kwao.

21. Utajiri wao nitautia mikononi mwa mataifa mengine,watu waovu wa dunia watauteka na kuutia najisi.

22. Uso wangu nitaugeuzia mbali naoili walitie najisi hekalu langu.Wanyanganyi wataingia humo ndani na kulitia najisi.

23. Tengeneza mnyororo.Kwa kuwa nchi imejaa makosa ya jinai ya umwagaji damuna mji umejaa dhuluma kupindukia,

24. nitayaleta mataifa mabaya sananao watazimiliki nyumba zao. Kiburi chao nitakikomesha,na mahali pao pa ibada patatiwa unajisi.

25. Uchungu mkali utakapowajia,watatafuta amani, lakini haitapatikana.

26. Watapata maafa mfululizo;nazo habari mbaya zitafuatana.Watamwomba nabii maono.Makuhani hawatakuwa na sheria yoyote;na wazee watakosa shauri la kuwapatia.

27. Mfalme ataomboleza,mkuu atakata tamaana watu watatetemeka kwa hofu.Nitawatenda kadiri ya mienendo yao,nitawahukumu kama nilivyowahukumu wengine.Ndipo watakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.”

Kusoma sura kamili Ezekieli 7