Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 31:8-15 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Miongoni mwa mierezi ya bustanini mwa Mungu,hakuna mti uliolingana nao,wala misonobari haikulingana na matawi yake,mibambakofi haikuwa na matawi kama yake,hata mti wowote wa bustani ya Munguhaukulingana nao kwa uzuri.

9. Mimi niliufanya kuwa mzurikwa matawi yake mengi;ulionewa wivu na miti yote ya Edeniiliyokuwa katika bustani ya Mungu.

10. “Kwa hiyo, mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Kwa sababu wewe ulirefusha kimo chake na kukiinua kilele chake kati ya matawi makubwa, ukajivunia urefu wake,

11. nitautia mikononi mwa mkuu kati ya mataifa. Yeye, atauadhibu. Nimeutupilia mbali kadiri ya uovu wake.

12. Watu wa mataifa mengine katili kupindukia, wataukata na kuubwaga chini na kuuacha. Matawi yake yataanguka chini mlimani na kila mahali mabondeni; yatavunjika na kutapakaa chini katika magenge yote. Watu wote wataondoka kivulini mwake na kuuacha.

13. Ndege wote watatua juu ya mabaki yake na wanyama wote wa porini watakanyaga matawi yake.

14. Hayo yameupata ili mti wowote ulio mahali penye maji usiweze kurefuka tena kiasi hicho wala kukifikisha kilele chake mawinguni. Mti wowote unaonyweshwa maji usiweze tena kufikia urefu huo. Kwa maana kila kitu mwisho wake ni kifo; hali kadhalika na watu. Wote watashiriki hali yao washukao shimoni kwa wafu.

15. “Kwa hiyo mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Siku ileile mwerezi ulipofika kuzimu nilitandaza giza nene juu yake nikaufunika; mito yake niliikausha na mtiririko wa maji yake mengi nikaukomesha. Nayo Lebanoni niliiweka gizani kwa ajili yake, na miti yote msituni ikazirai kwa ajili yake.

Kusoma sura kamili Ezekieli 31