Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 27:8-15 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Watu wa Sidoni na Arvadiwalikuwa wapiga makasia wako.Wenye hekima wako walikuwa ndaniwakifanya kazi kama wanamaji.

9. Wazee wa Gebali na mafundi waowalikuwa kwako kuziba nyufa zako.Mabaharia waliokuwa wakipitia kwakowalifanya biashara nawe.

10. Watu kutoka Persia, Ludi na Putiwalijiunga katika jeshi lako;walirundika kwenye kambi zao za jeshingao zao na kofia zao.Wanajeshi hao walikupatia fahari.

11. Watu wa Arvadi na wa Hele na jeshi lao walilinda kuta zako pande zote, nao watu wa Gamadi walilinda minara yako. Walitundika ngao zao kwenye kuta zako pande zote, na hivyo wakaukamilisha uzuri wako.

12. Watu wa Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mwingi na wa kila namna. Walitoa fedha, chuma, bati, na risasi kupata bidhaa zako.

13. Watu wa Yavani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, wakakupatia watumwa na vifaa vya shaba wapate bidhaa zako.

14. Bidhaa zako uliziuza huko Beth-togarma ili kujipatia farasi wa mizigo na wa vita, ngamia na nyumbu.

15. Watu wa Dedani walifanya biashara nawe. Nchi nyingi za pwani zilikuwa masoko yako maalumu. Watu wake walikuletea pembe za ndovu na mipingo kulipia bidhaa zako.

Kusoma sura kamili Ezekieli 27