Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 27:16-22 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Watu wa Edomu walifanya biashara nawe kwa sababu ya wingi wa bidhaa zako. Kwa kupata bidhaa zako walikupa akiki, vitambaa vya urujuani, vitambaa vilivyonakshiwa, kitani safi, matumbawe na yakuti.

17. Hata watu wa Yuda na Israeli walifanya biashara nawe; walikupa ngano, zeituni, tini za mwanzoni, asali, mafuta na marhamu kulipia bidhaa zako.

18. Watu wa Damasko walifanya biashara nawe kwa sababu ya wingi wa bidhaa zako; walikupa divai kutoka Helboni na sufu nyeupe.

19. Vedani na Yavani walisafirisha bidhaa zako toka Uzali; hata chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai ili kupata bidhaa zako.

20. Watu wa Dedani walifanya biashara nawe kwa kukupatia matandiko ya farasi.

21. Waarabu na wakuu wote wa nchi ya Kedari walikuwa wachuuzi wako wakuu katika biashara ya wanakondoo, kondoo madume na mbuzi.

22. Wachuuzi wa Sheba na wa Rama walifanya biashara nawe; walikuletea viungo vya chakula, vito vya thamani na dhahabu kujipatia bidhaa zako safi.

Kusoma sura kamili Ezekieli 27