1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:
2. “Sasa ewe mtu, imba utenzi huu wa maombolezo juu ya mji wa Tiro,
3. mji ule kando ya bahari, unaofanya biashara na mataifa ya pwani. Uambie: Bwana Mwenyezi-Mungu asema hivi:Ewe Tiro, wewe umejigambau mzuri kwelikweli!
4. Mipaka yako imeenea kwelikweli!Umejengwa kama meli nzuri.
5. Wajenzi wako walitumia misonobari kutoka Senirikupasua mbao zako zote;walichukua mierezi kutoka Lebanonikukutengenezea mlingoti.