Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 17:2-8 Biblia Habari Njema (BHN)

2. “Wewe mtu! Tega kitendawili, uwaambie fumbo Waisraeli.

3. Waambie kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Kulikuwa na tai mmoja mkubwa sanaaliyekuwa na mabawa makubwa,yenye manyoya marefu mengiyenye rangi za kila aina.Tai huyo aliruka mpaka mlimani Lebanoni,akatua juu ya kilele cha mwerezi;

4. akakwanyua tawi lake la juu zaidi,akalipeleka katika nchi ya wafanyabiashara,akaliweka katika mji wao mmoja.

5. Kisha akachukua mmea mchanga nchini Israeli,akaupanda katika ardhi yenye rutubaambako kulikuwa na maji mengi.

6. Mmea ukakua ukawa mzabibuwa aina ya mti utambaao;matawi yake yakamwelekea,na mizizi yake ikatanda chini yake.Mzabibu ukachipua matawi na majani mengi.

7. Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa;alikuwa na mabawa makubwa ya manyoya mengi.Basi, ule mzabibu ukamtandia mizizi yake,ukamwelekezea matawi yake,ili aumwagilie maji.

8. Mzabibu ulikuwa umetolewa kitaluni mwakeukapandikizwa penye udongo mzuri na maji mengi,ili upate kutoa matawi na kuzaa matundauweze kuwa mzabibu mzuri sana!

Kusoma sura kamili Ezekieli 17