Agano la Kale

Agano Jipya

Esta 4:6-10 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Hathaki alimwendea Mordekai uwanjani, mbele ya lango la ikulu.

7. Mordekai akamsimulia Hathaki yote yaliyokuwa yamempata, na kiasi kamili cha fedha ambayo Hamani alikuwa ameahidi kulipa katika hazina ya mfalme kama Wayahudi wote wangeangamizwa.

8. Alimpa pia nakala moja ya tangazo lililokuwa limetolewa mjini Susa kuhusu kuangamizwa kwa Wayahudi, akamwomba amchukulie Esta, amweleze hali ilivyo, na kumwambia aende kumsihi mfalme na kumwomba awahurumie Wayahudi, watu wake Esta.

9. Hathaki akaenda akamweleza Esta yote aliyosema Mordekai.

10. Naye Esta akamwambia Hathaki arudi akamwambie Mordekai,

Kusoma sura kamili Esta 4