Agano la Kale

Agano Jipya

Danieli 2:17-23 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Kisha, Danieli akarudi nyumbani, akawajulisha wenzake Hanania, Mishaeli na Azaria jambo hilo.

18. Aliwaambia wamwombe Mungu wa mbinguni awaonee huruma kuhusu fumbo hilo, ili wao wasiangamie pamoja na wenye hekima wengine wa Babuloni.

19. Ndipo Danieli alipofunuliwa fumbo hilo usiku katika maono. Naye Danieli akamshukuru Mungu wa mbinguni,

20. akasema,“Na litukuzwe milele na milele jina lake Mungu.Hekima na nguvu ni vyake.

21. Hubadilisha nyakati na majira,huwaondoa na kuwatawaza wafalme.Wenye busara huwapa hekima,wenye maarifa huwaongezea ufahamu.

22. Hufunua siri na mafumbo,ajua kilichoko gizani,mwanga wakaa kwake.

23. Kwako, ee Mungu wa wazee wangu,natoa shukrani na kukusifu,maana umenipa hekima na nguvu,umetujulisha kile tulichokuomba,umetujulisha kile kisa cha mfalme.”

Kusoma sura kamili Danieli 2