Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9

Agano la Kale

Agano Jipya

Amosi 4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Sikilizeni neno hili,enyi wanawake ng'ombe wa Bashanimlioko huko mlimani Samaria;nyinyi mnaowaonea wanyonge,mnaowakandamiza maskini,na kuwaambia waume zenu:“Tuleteeni divai tunywe!”Sikilizeni ujumbe huu:

2. Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu Mtakatifu nimeapa:“Tazama, siku zaja,ambapo watu watawakokoteni kwa kulabu,kila mmoja wenu kama samaki kwenye ndoana.

3. Mtaburutwa hadi ukutani palipobomolewa,na kutupwa nje.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.

Israeli haijajirekebisha bado

4. “Enyi Waisraeli,nendeni basi huko Betheli mkaniasi!Nendeni Gilgali mkalimbikize makosa yenu!Toeni sadaka zenu kila asubuhi,na zaka zenu kila siku ya tatu.

5. Toeni tambiko ya shukrani ya mikate iliyochachushwa.Tangazeni popote kwamba mmetoa kwa hiari;kwani ndivyo mnavyopenda kufanya!Mimi Bwana Mungu nimenena.

6. “Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna,nikasababisha ukosefu wa chakula popote.Hata hivyo hamkunirudia.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.

7. “Tena niliwanyima mvuamiezi mitatu tu kabla ya mavuno.Niliunyeshea mvua mji mmoja,na mji mwingine nikaunyima.Shamba moja lilipata mvua,na lingine halikupata, likakauka.

8. Watu wa miji miwili, mitatu wakakimbilia mji mwingine,wapate maji, lakini hayakuwatosha.Hata hivyo hamkunirudia.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.

9. “Niliwapiga pigo la ukame na ukungu;nikakausha bustani na mashamba yenu ya mizabibu;nzige wakala mitini na mizeituni yenu.Hata hivyo hamkunirudia.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.

10. “Niliwaleteeni ugonjwa wa taunikama ule nilioupelekea Misri.Niliwaua vijana wenu vitani,nikawachukua farasi wenu wa vita.Maiti zilijaa katika kambi zenu,uvundo wake ukajaa katika pua zenu.Hata hivyo hamkunirudia.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.

11. “Niliwaangusha baadhi yenu kwa maangamizikama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora.Wale walionusurika miongoni mwenu,walikuwa kama kijiti kilichookolewa motoni.Hata hivyo hamkunirudia.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.

12. “Kwa hiyo, enyi Waisraeli, nitawaadhibu.Na kwa kuwa nitafanya jambo hilo,kaeni tayari kuikabili hukumu yangu!”

13. Mungu ndiye aliyeifanya milima,na kuumba upepo;ndiye amjulishaye mwanadamu mawazo yake;ndiye ageuzaye mchana kuwa usiku,na kukanyaga vilele vya dunia.Mwenyezi-Mungu wa Majeshi ndilo jina lake!