Sura

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4
  5. 5
  6. 6
  7. 7
  8. 8
  9. 9

Agano la Kale

Agano Jipya

Amosi 2 Biblia Habari Njema (BHN)

Moabu

1. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Watu wa Moabu wametenda dhambi tena na tena,kwa hiyo sitaacha kuwaadhibu.Wamemkosea heshima marehemu mfalme wa Edomukwa kuichoma moto mifupa yakeili kujitengenezea chokaa!

2. Basi, nitaishushia moto nchi ya Moabu,na kuziteketeza kabisa ngome za mji wa Keriothi.Wanajeshi watakapopaza sauti zao na kupiga tarumbeta,watu wa Moabu watakufa katika makelele hayo ya vita.

3. Isitoshe, nitamuua mtawala wa Moabu,pamoja na viongozi wote wa nchi hiyo.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Yuda

4. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Watu wa Yuda wametenda dhambi tena na tena,kwa hiyo sitaacha kuwaadhibu.Wamepuuza sheria zangu,wala hawakufuata amri zangu.Wamepotoshwa na miungu ileile waliyoihudumia wazee wao.

5. Basi, nitaishushia moto nchi ya Yuda,na kuziteketeza kabisa ngome za Yerusalemu.”

Hukumu ya Mungu juu ya Israeli

6. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Waisraeli wametenda dhambi tena na tena,kwa hiyo sitaacha kuwaadhibu.Wamewauza watu waaminifukwa kuwa hawakuweza kulipa madeni yao;na kuwauza watu fukarawasioweza kulipa deni la kandambili.

7. Huwanyanyasa na kuwakandamiza wanyonge,na maskini huwabagua wasipate haki zao.Mtu na baba yake hulala na mjakazi yuleyule,hivyo hulitia unajisi jina langu takatifu.

8. Popote penye madhabahu,watu hulalia nguo walizotwaa kwa maskinikama dhamana ya madeni yao;na katika nyumba ya Mungu waohunywa divai waliyotwaa kwa wadeni wao.

9. “Hata hivyo, enyi watu wangu,kwa ajili yenu, niliwaangamiza kabisa Waamoriambao walikuwa wakubwa kama mierezi,wenye nguvu kama miti ya mialoni.Naam, niliwaangamiza, matawi na mizizi.

10. Niliwatoeni kutoka nchi ya Misri,nikawaongoza kupitia jangwani miaka arubaini,mpaka mkaichukua nchi ya Waamori kuwa yenu.

11. Niliwateua baadhi ya wana wenu wawe manabii,na baadhi ya vijana wenu wawe wanadhiri.Je, enyi Waisraeli,haya nisemayo si ya kweli?Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

12. Lakini nyinyi mliwafanya wanadhiri wanywe divai,na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.

13. “Sasa basi, nitawagandamiza mpaka chini,kama gari lililojaa nafaka.

14. Hata wapiga mbio hodari hawataweza kutoroka;wenye nguvu wataishiwa nguvu zao,na askari watashindwa kuyaokoa maisha yao.

15. Wapiga upinde vitani hawatastahimili;wapiga mbio hodari hawataweza kujiokoa,wala wapandafarasi hawatayanusurisha maisha yao.

16. Siku hiyo, hata askari hodariwatatimua mbio bila chochote.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”