Agano la Kale

Agano Jipya

2 Wafalme 19:22-35 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Je, uliyekuwa unamkashifu na kumdhihaki ni nani?Nani umemwinulia sautina kumkodolea macho kwa kiburi?Juu ya Mtakatifu wa Israeli!”

23. Kwa kuwatuma wajumbe wako umemkashifu Bwana,wewe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita,nimekwea vilele vya milimampaka kilele cha Lebanoni.Nimekata mierezi yake mirefu,na misonobari mizurimizuri;nimeingia mpaka ndani yakena ndani ya misitu yake mikubwa.

24. Nimechimba visimana kunywa maji mageninilikausha mito yote ya Misrikwa nyayo za miguu yangu.

25. ‘Je, hujasikia,kwamba nilipanga jambo hili tangu awali?Ninachotekeleza sasa nilikipanga zamani.’Nilikuweka uijenge miji yenye ngomekwa rundo la magofu.

26. Wakazi wake wakiwa wameishiwa nguvu,wametishika na kufadhaika,wamekuwa kama mimea ya shambani,kama majani yasiyo na nguvu.Kama majani yaotayo juu ya paa;yakaukavyo kabla ya kukua.

27. Najua kuketi kwako,na kuamka kwakonako kuingia kwako;nayo mipango yako dhidi yangu.

28. Kwa vile umefanya mipango dhidi yanguna nimeusikia ufidhuli wako,nitatia ndoana yangu puani mwako,na lijamu yangu kinywani mwako.Nitakurudisha njia ileile uliyojia.”

29. Kisha Isaya akamwambia mfalme Hezekia, “Na hii ndio itakuwa ishara kwako Hezekia: Mwaka huu na mwaka ujao mtakula kinachomea chenyewe bila kupandwa. Lakini katika mwaka wa tatu mtapanda na kuvuna mavuno; mtapanda mizabibu na kula matunda yake.

30. Wale watakaobaki katika ukoo wa Yuda wataongezeka na kuwa wengi kama vile mti unavyotoa mizizi yake udongoni na kuzaa matunda juu.

31. Maana kutakuwako watu watakaosalia huko Yerusalemu; naam, huko mlimani Siyoni kutakuwako watu wachache watakaosalimika; maana Mwenyezi-Mungu amedhamiria kukamilisha hayo.

32. “Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi juu ya mfalme wa Waashuru: ‘Hataingia katika mji huu wala kuupiga mshale wala kuujia kwa ngao wala kuuzingira.

33. Atarudi kwa njia ileile aliyoijia na wala hataingia katika mji huu,’ ndivyo asemavyo Mwenyezi-Mungu.

34. ‘Naam, kwa ajili ya heshima yangu mimi na kwa ajili ya mtumishi wangu Daudi nitaulinda na kuokoa mji huu.’”

35. Basi, usiku huo malaika wa Mwenyezi-Mungu aliingia kambini mwa Waashuru na kuwaua watu laki moja. Kulipopambazuka watu wakaamka, hao wote walionekana wakiwa maiti.

Kusoma sura kamili 2 Wafalme 19