Agano la Kale

Agano Jipya

2 Wafalme 19:12-25 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Je, miungu ya mataifa iliokoa Gozani, Harani, na Resefu na Waedeni waliokaa Telasari, mataifa ambayo babu zangu waliyaangamiza?

13. Wako wapi wafalme wa Hamathi, Arpadi, Sefarvaimu, Hena na wa Iva?’”

14. Mfalme Hezekia alipokea barua kutoka kwa wajumbe na kuisoma. Kisha akaenda na kuingia katika nyumba ya Mwenyezi-Mungu, naye akaiweka mbele yake Mwenyezi-Mungu.

15. Halafu akamwomba Mwenyezi-Mungu akisema, “Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, unayekaa katika kiti cha enzi juu ya viumbe wenye mabawa, ni wewe tu uliye Mungu, unayetawala falme zote za ulimwengu. Wewe uliumba nchi na mbingu.

16. Ee Mwenyezi-Mungu, fumbua macho uone, tega sikio lako, uyasikie matusi yote ambayo Senakeribu amepeleka kukutukana wewe Mungu uliye hai.

17. Ee Mwenyezi-Mungu, ni kweli kwamba wafalme wa Ashuru wameangamiza mataifa na nchi zao.

18. Walitupa miungu yao motoni kwa sababu haikuwa miungu ya kweli, bali sanamu za miti na mawe zilizochongwa na mikono ya watu.

19. Sasa, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, nakusihi utuokoe makuchani mwa Senakeribu, falme zote za dunia zijue kwamba ni wewe peke yako, ee Mwenyezi-Mungu, uliye Mungu.”

20. Kisha Isaya, mwana wa Amozi akatuma ujumbe kwa Hezekia, akisema, “Hivi ndivyo anavyosema Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, ‘Nimesikia ombi lako kwangu kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru:’

21. Hili ndilo neno la Mwenyezi-Mungu alilosema kumhusu Senakeribu:Anakudharau, anakubeza binti Siyoni,anatikisa kichwa chake nyuma yako binti Yerusalemu.

22. Je, uliyekuwa unamkashifu na kumdhihaki ni nani?Nani umemwinulia sautina kumkodolea macho kwa kiburi?Juu ya Mtakatifu wa Israeli!”

23. Kwa kuwatuma wajumbe wako umemkashifu Bwana,wewe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita,nimekwea vilele vya milimampaka kilele cha Lebanoni.Nimekata mierezi yake mirefu,na misonobari mizurimizuri;nimeingia mpaka ndani yakena ndani ya misitu yake mikubwa.

24. Nimechimba visimana kunywa maji mageninilikausha mito yote ya Misrikwa nyayo za miguu yangu.

25. ‘Je, hujasikia,kwamba nilipanga jambo hili tangu awali?Ninachotekeleza sasa nilikipanga zamani.’Nilikuweka uijenge miji yenye ngomekwa rundo la magofu.

Kusoma sura kamili 2 Wafalme 19