38. wala msisahau agano nililofanya nanyi; msiiabudu miungu mingine, bali
39. mtaniabudu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, nami nitawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu.”
40. Lakini watu hao hawakusikiliza, bali waliendelea kutenda kama walivyofanya hapo awali.
41. Basi mataifa haya yalimwabudu Mwenyezi-Mungu, lakini pia yalitumikia sanamu zao za kusubu; na mpaka sasa hivi, wazawa wao wanaendelea kutenda hivyo kama walivyotenda babu zao.