Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 23:4-9 Biblia Habari Njema (BHN)

4. yeye ni kama mwanga wa asubuhi,jua linapochomoza asubuhi isiyo na mawingu;naam, kama mvua inayootesha majani ardhini’.

5. Hivyo ndivyo Mungu alivyoujalia ukoo wangu.Maana amefanya nami agano la kudumu milele;agano kamili na thabiti.Naye atanifanikisha katika matakwa yangu yote.

6. Lakini wasiomcha Munguwote ni kama miiba inayotupwa tu,maana haiwezi kuchukuliwa kwa mkono;

7. kuishika, lazima kutumia chuma au mpini wa mkuki.Watu hao wataangamizwa kabisa kwa moto.”

8. Yafuatayo ni majina ya mashujaa aliokuwa nao Daudi: Yosheb-bashebethi, Mtakmoni, aliyekuwa kiongozi wa wale watatu, yeye alipigana kwa mkuki wake, akaua watu 800 wakati mmoja.

9. Halafu aliyefuata miongoni mwa wale mashujaa watatu alikuwa Eleazari mwana wa Dodo, wa ukoo wa Mwahohi. Siku moja, Eleazari alikuwa pamoja na Daudi walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika kupigana vita. Waisraeli waliwakimbia Wafilisti.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 23