Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 22:6-13 Biblia Habari Njema (BHN)

6. kamba za kuzimu zilinizinga,mitego ya kifo ilinikabili.

7. “Katika taabu yangu, nilimwita Mwenyezi-Mungu;nilimwita Mungu wangu.Toka hekaluni mwake aliisikia sauti yangu,kilio changu kilimfikia masikioni mwake.

8. “Hapo, dunia ikatetemeka na kutikisika,misingi ya mbinguni ikayumbayumba na kuruka,kwani Mungu alikuwa amekasirika.

9. Moshi ulifuka kutoka puani mwake,moto uunguzao ukatoka kinywani mwake,makaa ya moto yalilipuka kutoka kwake.

10. Aliinamisha anga, akashuka chini;na wingu jeusi chini ya miguu yake.

11. Alipanda kiumbe chenye mabawa na kuruka,alionekana juu ya mabawa ya upepo.

12. Alijizungushia giza pande zote,kifuniko chake kilikuwa mawingu mazito na mkusanyiko wa maji.

13. Umeme ulimulika mbele yake,kulilipuka makaa ya moto.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 22