Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 22:41-51 Biblia Habari Njema (BHN)

41. Uliwafanya adui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.

42. Walitafuta msaada, lakini hapakuwa na wa kuwaokoa,walimlilia Mwenyezi-Mungu, lakini hakuwajibu.

43. Niliwatwanga na kuwaponda kama mavumbi ya nchi,nikawaponda na kuwakanyaga kama matope barabarani.

44. “Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu wangu,umenifanya mtawala wa mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.

45. Wageni walinijia wakinyenyekea,mara waliposikia habari zangu walinitii.

46. Wageni walikufa moyo;wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.

47. “Mwenyezi-Mungu yu hai!Asifiwe mwamba wangu!Atukuzwe Mungu wangu, mwamba wa wokovu wangu.

48. Yeye ameniwezesha kulipiza kisasina kuyatiisha mataifa chini yangu.

49. Ameniokoa kutoka adui zangu.Ee Mwenyezi-Mungu, ulinikuza juu ya wapinzani wanguna kunisalimisha mbali na watu wakatili.

50. “Kwa hiyo, nitakutukuza kati ya mataifa,ee Mwenyezi-Mungu, nitaliimbia sifa jina lako.

51. Mungu humjalia mfalme wake ushindi mkubwa;humwonesha fadhili zake huyo aliyemweka wakfu,naam, humfadhili Daudi na wazawa wake milele.”

Kusoma sura kamili 2 Samueli 22