40. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha adui chini yangu.
41. Uliwafanya adui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.
42. Walitafuta msaada, lakini hapakuwa na wa kuwaokoa,walimlilia Mwenyezi-Mungu, lakini hakuwajibu.
43. Niliwatwanga na kuwaponda kama mavumbi ya nchi,nikawaponda na kuwakanyaga kama matope barabarani.