Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 22:35-47 Biblia Habari Njema (BHN)

35. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.

36. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;msaada wako umenifanya mkuu.

37. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.

38. Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza,sikurudi nyuma mpaka wameangamizwa.

39. Niliwaangamiza, nikawaangusha chiniwasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.

40. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha adui chini yangu.

41. Uliwafanya adui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.

42. Walitafuta msaada, lakini hapakuwa na wa kuwaokoa,walimlilia Mwenyezi-Mungu, lakini hakuwajibu.

43. Niliwatwanga na kuwaponda kama mavumbi ya nchi,nikawaponda na kuwakanyaga kama matope barabarani.

44. “Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu wangu,umenifanya mtawala wa mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.

45. Wageni walinijia wakinyenyekea,mara waliposikia habari zangu walinitii.

46. Wageni walikufa moyo;wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.

47. “Mwenyezi-Mungu yu hai!Asifiwe mwamba wangu!Atukuzwe Mungu wangu, mwamba wa wokovu wangu.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 22