Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 22:35-41 Biblia Habari Njema (BHN)

35. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.

36. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;msaada wako umenifanya mkuu.

37. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.

38. Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza,sikurudi nyuma mpaka wameangamizwa.

39. Niliwaangamiza, nikawaangusha chiniwasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.

40. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha adui chini yangu.

41. Uliwafanya adui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 22