35. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.
36. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;msaada wako umenifanya mkuu.
37. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.
38. Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza,sikurudi nyuma mpaka wameangamizwa.
39. Niliwaangamiza, nikawaangusha chiniwasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.
40. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha adui chini yangu.
41. Uliwafanya adui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.