Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 22:23-41 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Nimeshika maagizo yake yote,sikuacha kufuata masharti yake.

24. Mbele yake sikuwa na hatia,nimejikinga nisiwe na hatia.

25. Mwenyezi-Mungu amenituza kadiri ya uadilifu wangu,yeye anajua usafi wangu.

26. “Wewe ni mwaminifu kwa walio waaminifu,mwema kwa wale walio wema.

27. Wewe ni mkamilifu kwa walio wakamilifu,lakini mkatili kwa watu walio waovu.

28. Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu,lakini wawaangalia wenye majivuno kuwaporomosha.

29. Ee Mwenyezi-Mungu, wewe u taa yangu,Mungu wangu, unayefukuza giza langu.

30. Kwa msaada wako, wakishambulia kikosi;wewe wanipa nguvu ya kuruka kuta zake.

31. Anachofanya Mungu hakina dosari!Ahadi ya Mwenyezi-Mungu ni ya kuaminika;yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia.

32. “Nani aliye Mungu isipokuwa Mwenyezi-Mungu?Nani aliye mwamba wa usalama ila Mungu wetu?

33. Mungu huyu ndiye kimbilio langu imara,na ameifanya njia yangu iwe salama.

34. Ameiimarisha miguu yangu kama ya paa,na kuniweka salama juu ya vilele.

35. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.

36. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;msaada wako umenifanya mkuu.

37. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.

38. Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza,sikurudi nyuma mpaka wameangamizwa.

39. Niliwaangamiza, nikawaangusha chiniwasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.

40. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha adui chini yangu.

41. Uliwafanya adui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 22