Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 22:19-24 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Walinivamia nilipokuwa taabuni,lakini Mwenyezi-Mungu alikuwa kinga yangu.

20. Alinileta, akaniweka mahali pa usalama,alinisalimisha, kwani alipendezwa nami.

21. “Mwenyezi-Mungu alinipa tuzo kadiri ya uadilifu wangu;alinituza kwa vile mikono yangu haina hatia.

22. Maana, nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu,wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.

23. Nimeshika maagizo yake yote,sikuacha kufuata masharti yake.

24. Mbele yake sikuwa na hatia,nimejikinga nisiwe na hatia.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 22