Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 22:16-30 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Mwenyezi-Mungu alipowakemea,kutokana na pumzi ya puani mwake,vilindi vya bahari vilifunuliwa,misingi ya dunia ikaonekana.

17. “Mungu alinyosha mkono wake toka juu, akanichukua,kutoka kwenye maji mengi alininyanyua.

18. Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,aliniokoa kutoka kwa hao walionichukiamaana walikuwa na nguvu nyingi kunishinda.

19. Walinivamia nilipokuwa taabuni,lakini Mwenyezi-Mungu alikuwa kinga yangu.

20. Alinileta, akaniweka mahali pa usalama,alinisalimisha, kwani alipendezwa nami.

21. “Mwenyezi-Mungu alinipa tuzo kadiri ya uadilifu wangu;alinituza kwa vile mikono yangu haina hatia.

22. Maana, nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu,wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.

23. Nimeshika maagizo yake yote,sikuacha kufuata masharti yake.

24. Mbele yake sikuwa na hatia,nimejikinga nisiwe na hatia.

25. Mwenyezi-Mungu amenituza kadiri ya uadilifu wangu,yeye anajua usafi wangu.

26. “Wewe ni mwaminifu kwa walio waaminifu,mwema kwa wale walio wema.

27. Wewe ni mkamilifu kwa walio wakamilifu,lakini mkatili kwa watu walio waovu.

28. Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu,lakini wawaangalia wenye majivuno kuwaporomosha.

29. Ee Mwenyezi-Mungu, wewe u taa yangu,Mungu wangu, unayefukuza giza langu.

30. Kwa msaada wako, wakishambulia kikosi;wewe wanipa nguvu ya kuruka kuta zake.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 22