Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 22:12-18 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Alijizungushia giza pande zote,kifuniko chake kilikuwa mawingu mazito na mkusanyiko wa maji.

13. Umeme ulimulika mbele yake,kulilipuka makaa ya moto.

14. Mwenyezi-Mungu alinguruma kutoka mbinguni,Mungu Mkuu akatoa sauti yake.

15. Aliwalenga adui mishale, akawatawanya,alirusha umeme, akawatimua.

16. Mwenyezi-Mungu alipowakemea,kutokana na pumzi ya puani mwake,vilindi vya bahari vilifunuliwa,misingi ya dunia ikaonekana.

17. “Mungu alinyosha mkono wake toka juu, akanichukua,kutoka kwenye maji mengi alininyanyua.

18. Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,aliniokoa kutoka kwa hao walionichukiamaana walikuwa na nguvu nyingi kunishinda.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 22