Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 22:10-14 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Aliinamisha anga, akashuka chini;na wingu jeusi chini ya miguu yake.

11. Alipanda kiumbe chenye mabawa na kuruka,alionekana juu ya mabawa ya upepo.

12. Alijizungushia giza pande zote,kifuniko chake kilikuwa mawingu mazito na mkusanyiko wa maji.

13. Umeme ulimulika mbele yake,kulilipuka makaa ya moto.

14. Mwenyezi-Mungu alinguruma kutoka mbinguni,Mungu Mkuu akatoa sauti yake.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 22