Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 21:19-22 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Kulitokea tena mapigano na Wafilisti huko Gobu. Naye Elhanani mwana wa Yaareo-regimu, Mbethlehemu, alimuua Goliathi Mgiti, ambaye mpini wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumanguo.

20. Baadaye kulitokea tena vita huko Gathi ambako kulikuwa na mtu mmoja alikuwa mkubwa kwa kimo, na mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake vidole ishirini na vinne. Yeye pia alikuwa mzawa wa majitu.

21. Alipowadhihaki Waisraeli, Yonathani mwana wa Shimei, nduguye Daudi, alimuua.

22. Hao wanne walikuwa wazawa wa majitu huko Gathi, nao waliuawa na Daudi pamoja na watumishi wake.

Kusoma sura kamili 2 Samueli 21