Agano la Kale

Agano Jipya

2 Samueli 1:22-27 Biblia Habari Njema (BHN)

22. “Upinde wa Yonathani kamwe haukurudi nyuma,upanga wa Shauli kamwe haukurudi bure,daima ziliua wengi.Naam, ziliua mashujaa.

23. “Shauli na Yonathani,watu wa ajabu na wakupendeza.Maishani na kifoni hawakutengana.Walikuwa wepesi kuliko tai,naam, wenye nguvu kuliko simba.

24. “Wanawake wa Israeli, mlilieni Shauli!Aliwavika mavazi mekundu ya fahari,aliyatarizi mavazi yenu kwa dhahabu.

25. “Jinsi gani mashujaa walivyoanguka!Wamekufa wakiwa katika mapambano.Yonathani analala,akiwa ameuawa milimani.

26. Nasikitika kwa ajili yako, ndugu yangu Yonathani.Umekuwa kwangu daima mtu wa kupendeza,pendo lako kwangu limekuwa la ajabu,la ajabu kuliko la mwanamke.

27. “Jinsi gani mashujaa wameanguka,na silaha zao zimeachwa, hazina kazi.”

Kusoma sura kamili 2 Samueli 1