Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 34:19-21 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Mfalme aliposikia maneno ya sheria alirarua mavazi yake.

20. Ndipo alipomwamuru Hilkia, Ahikamu mwana wa Shafani, Abdoni mwana wa Mika, katibu Shafani na Asaya, mtumishi wa mfalme, akisema,

21. “Nendeni mkatafute shauri kutoka kwa Mwenyezi-Mungu kwa niaba yangu na watu ambao wamebaki katika Israeli na Yuda, kuhusu maneno yaliyomo katika kitabu kilichopatikana. Kwa sababu ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu imetuangukia, maana babu zetu hawakushika neno la Mwenyezi-Mungu, wala kufanya yaliyoandikwa humo.”

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 34