Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 3:2-4 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Mfalme Solomoni alianza ujenzi wa hekalu mnamo mwezi wa pili wa mwaka wa nne wa utawala wake.

3. Vipimo alivyotumia Solomoni katika ujenzi wa nyumba ya Mungu, vilikuwa kadiri ya vipimo vya awali, urefu mita 27 na upana mita 9.

4. Chumba cha sehemu ya kuingilia kilikuwa na urefu wa mita 9, sawa na upana wa nyumba hiyo, na kimo chake mita 54. Kuta zake zilifunikwa kwa dhahabu safi upande wa ndani.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 3