Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 14:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwishowe, Abiya alifariki na kuzikwa katika mji wa Daudi na Asa mwanawe akatawala mahali pake. Wakati wa Asa, kulikuwa na amani nchini kwa muda wa miaka kumi.

2. Asa alitenda yaliyokuwa mazuri na mema mbele ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wake.

3. Aliondoa nchini madhabahu za kigeni na mahali pa kuabudia miungu mingine, akabomoa minara na kuzikatakata sanamu za Ashera.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 14