Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 11:8-14 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Gathi, Maresha, Zifu,

9. Adoraimu, Lakishi, Azeka,

10. Sora, Ayaloni na Hebroni. Miji hiyo yenye ngome imo Yuda na Benyamini.

11. Aliziimarisha ngome hizo na humo ndani akaweka makamanda na maghala ya vyakula, mafuta na divai.

12. Ndani ya kila mji, aliweka ngao na mikuki, na kuifanya miji hiyo kuwa imara sana. Yuda na Benyamini zikawa chini ya mamlaka yake.

13. Makuhani na Walawi wote waliokuwa wanaishi kote nchini Israeli, walimwendea kutoka maeneo yao.

14. Walawi waliyaacha malisho yao, na maeneo yao mengine kwa sababu Yeroboamu na wanawe waliwakataza kumtumikia Mwenyezi-Mungu kama makuhani wa Mwenyezi-Mungu.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 11