Agano la Kale

Agano Jipya

2 Mambo Ya Nyakati 11:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Rehoboamu alipofika Yerusalemu, alikusanya askari stadi180,000 wa makabila ya Yuda na Benyamini, apate kupigana na Israeli, ili ajirudishie huo ufalme.

2. Lakini ujumbe wa Mungu ulimjia Shemaya mtu wa Mungu, kusema:

3. “Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni, mfalme wa Yuda na Waisraeli wote katika Yuda na Benyamini ya kwamba

4. mimi Bwana nasema, ‘Msiende wala msipigane na ndugu zenu. Rudini kila mtu nyumbani kwake, maana hayo yaliyotokea ni kama nilivyopanga.’” Basi wakatii ujumbe wa Mwenyezi-Mungu, wakarudi nyumbani, wala hawakwenda kupigana na Yeroboamu.

5. Rehoboamu alikaa Yerusalemu na akajenga ngome na kuiimarisha miji ifuatayo iliyokuwa nchini Yuda:

6. Bethlehemu, Etamu, Tekoa,

7. Beth-suri, Soko, Adulamu,

8. Gathi, Maresha, Zifu,

9. Adoraimu, Lakishi, Azeka,

10. Sora, Ayaloni na Hebroni. Miji hiyo yenye ngome imo Yuda na Benyamini.

Kusoma sura kamili 2 Mambo Ya Nyakati 11