Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wafalme 7:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Msingi ulikuwa wa mawe ya thamani na makubwa yenye urefu wa mita 3.5, na upana mita 4.5.

11. Sehemu za juu zilijengwa kwa mawe mengine yaliyochongwa kwa vipimo maalumu, na kwa mbao za mierezi.

12. Ua wa nyumba ya mfalme ulikuwa na kuta zenye safu moja ya mbao za mierezi na safu tatu za mawe ya kuchongwa kila moja; ndivyo ilivyokuwa hata kwa ua wa ndani wa nyumba ya Mwenyezi-Mungu na kwa ukumbi wa nyumba.

13. Kisha mfalme Solomoni alimwita Hiramu kutoka Tiro.

Kusoma sura kamili 1 Wafalme 7