Agano la Kale

Agano Jipya

1 Wafalme 11:39-43 Biblia Habari Njema (BHN)

39. Kutokana na hayo, nitawaadhibu wazawa wa Daudi, lakini si daima.”

40. Kwa sababu hiyo, Solomoni alijaribu kumuua Yeroboamu; lakini Yeroboamu akakimbilia Misri kwa Shishaki mfalme wa Misri, akakaa huko mpaka Solomoni alipofariki.

41. Mambo mengine ya Solomoni, yote aliyotenda na hekima yake, yameandikwa katika Kitabu cha Matendo ya Solomoni.

42. Kwa muda wa miaka arubaini, Solomoni aliitawala nchi yote ya Israeli; makao yake yakiwa Yerusalemu.

43. Hatimaye, Solomoni alifariki, akazikwa katika mji wa baba yake Daudi. Rehoboamu, mwanawe Solomoni, akatawala mahali pake.

Kusoma sura kamili 1 Wafalme 11