Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 7:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Wana wa Isakari walikuwa wanne: Tala, Pua, Yashubu na Shimroni.

2. Wana wa Tola walikuwa: Uzi, Refaya, Yerieli, Yamai, Ibsamu na Shemueli. Hao walikuwa wakuu wa jamaa za koo za Tola na watu mashujaa sana wa vita nyakati zao. Idadi ya wazawa wao siku za mfalme Daudi ilikuwa 22,600.

3. Uzi alikuwa na mwana mmoja, jina lake Izrahia. Na wana wa Izrahia walikuwa Mikaeli, Obadia, Yoeli na Ishia, jumla wanne, na wote walikuwa wakuu wa jamaa.

4. Kwa vile ambavyo wake na watoto wao walikuwa wengi sana, mliweza kupatikana vikosi vya wanajeshi 36,000 kutokana na wazawa wao.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 7