Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 4:22-31 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Yokimu na watu walioishi katika mji wa Kozeba; na Yoashi na Sarafi waliotawala huko Moabu na wakarejea Lehemu. (Taarifa hizi ni za zamani sana.)

23. Hawa ndio wafinyanzi walioishi katika miji ya Netaimu na Gedera, wakimhudumia mfalme.

24. Simeoni alikuwa na wana watano: Nemueli, Yamini, Yaribu, Zera na Shauli.

25. Mwana wa Shauli alikuwa Shalumu; Shalumu alimzaa Mibsamu na Mibsamu akamzaa Mishma.

26. Mishma alimzaa Hamueli, aliyemzaa Zakuri, na Zakuri akamzaa Shimei.

27. Shimei alikuwa na wana kumi na sita na binti sita, lakini ndugu zake hawakuwa na wana wengi, na jamii yake pia haikuongezeka kama kabila la Yuda.

28. Miji walimokuwa wakiishi ilikuwa Beer-sheba, Molada, Hasar-shuali,

29. Bilha, Ezemu, Toladi;

30. Bethueli, Horma, Siklagi,

31. Beth-markabothi, Hazar-susimu, Beth-biri na Shaaraimu. Hiyo ndiyo miji yao mpaka wakati wa utawala wa mfalme Daudi.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 4