Agano la Kale

Agano Jipya

1 Mambo Ya Nyakati 4:11-17 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Kelubu, nduguye Shuha, alimzaa Mehiri na Mehiri akamzaa Eshtoni.

12. Eshtoni alikuwa na wana watatu: Beth-rafa, Pasea na Tehina. Tehina alikuwa mwanzilishi wa mji wa Ir-nahashi. Wazawa wa watu hawa waliishi Reka.

13. Wana wa Kenazi walikuwa: Othnieli na Seraya; na wana wa Othnieli walikuwa Hathathi na Meonothai.

14. Meonothai alimzaa Ofra. Seraya alimzaa Yoabu, mwanzilishi wa Bonde la Mafundi, lililopewa jina hilo kwa sababu wote waliokuwa humo walikuwa mafundi stadi.

15. Kalebu mwana wa Yefune alikuwa na wana watatu: Iru, Ela na Naamu. Na mwana wa Ela alikuwa Kenazi.

16. Wana wa Yehaleli walikuwa Zifu, Zifa, Tiria na Asareli.

17. Wana wa Ezra walikuwa Yetheri, Meredi, Eferi na Yaloni. Meredi alimwoa Bithia, bintiye Farao, na hawa ndio wana aliomzalia Meredi: Miriamu, Shamai na Ishba, mwanzilishi wa mji wa Eshtemoa.

Kusoma sura kamili 1 Mambo Ya Nyakati 4